0657128567

Mwanza Tanzania,

Karibu Sana Kwenye Mtandao huu Wa Shule Tanzania

Showing posts with label TENGENEZA PESA KWA MTANDAO. Show all posts
Showing posts with label TENGENEZA PESA KWA MTANDAO. Show all posts

Thursday, February 22, 2018

MAMBO NANE (8) MUHIMU SANA YA KUFAHAMU KABLA YA KUTENGENEZA BATIKI.

Habari rafiki yangu, naamini unaendelea vizuri na mapambano ya kuboresha maisha yako.

Kama ilivyo kawaida yangu nakufunulia fursa mbalimbali ambazo ukiamua kuchukua hatua unaweza kubadili maisha yako kabisa. Cha msingi sana ni kuchukua hatua.

Leo nakuletea fursa ya kutengeneza batiki, fursa ambayo si wengi sana wanaijua kwa maana ya jinsi ya kutengeneza, hata kama watu wanajua kutengeneza bado hawachukui hatua na kufanya fursa hii kuwa ya wachache na imewatajirisha wengi sana na wengine maisha yao yamebadilika kabisa.

Nisikuchoshe sana ndugu, leo hii nakuletea list ya vitu muhimu au mambo manane (8) ya muhimu kuyajua kabla ya kuanza kutengeneza batiki yenye ubora wa hali ya juu. Vitu hivyo ni:-

MAHITAJI:
1.Vibao vyenye urembo mbalimbali.
2.Sponji zenye urembo mbalimbali.
3.Brash kubwa/ndogo.
4.Meza kubwa yenye urefu wa mita moja mpaka mbili.
5.Sufuria.
6.Vitambaa
7. Jiko.

MADAWA:
8.Sodium hydrosulphate.
9.Caustic soda
10.Mshumaa.

KAZI ZAKE:
1.Sodium hydrosulphate ni kuimarisha rangi isichuje,kama itachanganywa na caustic soda.Madawa haya huwa kazi yake ni moja lakini ikikosekana moja nyingine haifanyi kazi.
2.Kazi ya mshumaa ni kuweka urembo kwenye nguo au kwenye vitambaa kwa kutumia vibao au sponji zenye urembo wa tembo,twiga,matunda au aina yoyote ya urembo unayotaka mtengenezaji.

Zifuatazo ni picha za baadhi ya batiki ambazo ninatengeneza na kuwauzia wateja wangu.

















Je unatamani kujua kutengeneza batiki?? Hii ni miongoni mwa fursa zilizojificha kabisa na watu hawazioni na hata kama wanaziona hawachukui hatua yoyote, kama unasoma makala hii na unasikia moyoni unatamani kujua jinsi ya kutengeneza batiki hizi basi naamini ndani ya muda mfupi unaenda kuwa mtu mwingine kabisa.

Inawezekana kabisa unajiuliza kuhusu mtaji inagharimu kiasi gani, nataka nikutoe hofu, mtaji wake ni kiasi kidogo saaaana ambacho huwezi kuamini, na utajiuliza kwa nini watu hawafanyi biashara hii kwa wingi na wakati mtaji ni kiasi kidoooooogo sana, nimeshasema sababu hapo juu ni kwamba watanzania wengi hatupendi kujishughulisha, tunapenda kukaa vijiweni kulalamika maisha magumu tu na kuzungumzia maisha ya watu. Ninaamini baada ya kusoma makala hii utakwenda kuchukua hatua mara moja.

Nina habari njema kwa wewe ambaye umependa kujifunza mradi huu.

Kama uko serious na unataka kujifunza jinsi ya kutengemeza batiki basi nimekuandalia kozi maalumu kwa ajili yako.
Kozi hiyo itakufundisha kwa kina, hatua kwa hatua jinsi ya kutengeneza batiki yenye mikunjo/michoro mbalimbali ya kupendeza machoni pa watu.

Kozi hiyo itakuwa kwa njia ya VIDEO ambayo itakusaidia kuangalia kwa vitendo jinsi tunavyokunja mikunjo hiyo na kuweka rangi mbalimbali.

Je uko tayari???

Kama uko tayari niandikie ujumbe whatsapp 0717375782 kwamba uko tayari kujifunza BATIKI kwa njia hiyo kisha nitakuingiza darasani. KARIBU SANA.

Najua bado unajiuliza mtaji ni shilingi ngapi???? Najua vijana wengi tukitaka kuanza mradi flani tunawaza sana kuhusu mitaji. Nataka nikwambie kwa mradi huu hata sh. 15,000/- unaweza kutengeneza batiki nzuri na watu wakabaki kukushangaa. Pia utakuwa unajiuliza nitatoa wapi malighafi???? nataka nikutoe hofu, Tanzania sasa ni ndogo sana, kama hutapata sehemu au mkoa uliopo tutakutumia popote ulipo ilimradi tu utimize ndoto zako. Usiogope, chukua hatua sasa, natamani sana kukuona darasani.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako;

Pius J. Muliriye
0717375782 | whatsapp tu.
0754745798 | meseji tu (usipige)
piusjustus28@gmail.com
www.piusjustus.com

Sunday, April 2, 2017

ZIJUE MBINU ZA JINSI YA KUFANYA BIASHARA MTANDAONI.


Angalia picha hii vizuri na ujifunze kitu...




Najua kuna watu wengi wanatamani kufanya biashara mtandaoni kama hapa facebook na watengeneze pesa, na nimeona watu wengi wakipost picha za bidhaa zao kwenye wall zao. Lakini je...umeshawahi kupata wateja kama ulivyotaka? Au watu wameishia kulike picha za bidhaa zako tu na kuondoka?

Umeshawahi kujiuliza kwanini bidhaa yako watu hawaichangamkii? Tatizo si kwamba bidhaa yako ni mbaya, tatizo hauko serious na biashara yako.

Mwanzoni nilifanya hivyo nilivyomaliza kuandika kitabu changu na nikapost kwenye wall yangu ya facebook lakini watu waliishia kulike na kunipongeza na hakuna aliyenunua kabisa kwa zaidi ya mwezi mzima mpaka nikaona nimepoteza nguvu zangu bure.

Niliamua kufanya utafiti wa jinsi gani ya kuwafanya watu waipende bidhaa yangu na hatimaye wawe wateja wangu.

Niligundua kitu muhimu sana katika hatua za kufanya biashara mtandaoni.
"Watu hawana shida na bidhaa yako, watu wanataka kujua bidhaa yako itawasaidiaje"

Hiyo ndiyo siri kubwa sana katika kufanya biashara mtandaoni.

Kitu kingine ambacho watu wengi hawapendi kukifanya ni kuogopa gharama!!! Watu hawapendi kulipia matangazo yao mtandaoni aidha kwa kujua au kwa kutokujua..

Ukiangalia picha hiyo utagundua kuwa nililipa gharama flani ili kuwafikia wateja niliokuwa nahitaji.....na niliuza kitabu changu kuzidi gharama niliyoitumia kulipia tangazo hilo.

Hiyo ni page yangu ya biashara ya facebook inayoitwa THINK BIG START SMALL, ina viewers 3000 lakini baada ya kulipia tangazo moja la kitabu changu nikapata watu 8,111 na kati ya hao walinunua bidhaa hiyo na hapo ndipo nilipogundua kuwa kuna wateja wengi tunashindwa kuwagikia kwa kukosa maarifa na kuogopa gharama.

Jiulize uko tayari kulipa gharama ili uuze? Au hauko tayari na uendelee kukaa na bidhaa yako?

Nakuhakishia kama unauza nguo, unaweza ukauza mpaka mikoani bila shida yoyote, kama unauza handbags, wallets, n.k unaweza ukauza mpaka ukashangaa!!! Cha msingi ni kutengeneza idadi ya watu wengi kadri uwezavyo kwenye page yako ya facebook(soko lako) ...na hii ni lazima ugharamie!!

Kama unahitaji kuwa mfanyabiashara mtandaoni unatakiwa uwe na vitu vifuatavyo;

1. Facebook page(hii ni tofauti na hiyo akaunti yako unayopost picha zako ukiwa na mpenzi wako au ukiwa beach unaogelea)

2. Blog (hii utaitumia kuelezea bidhaa zako ulizonazo, na ndipo utaweka picha nyingi za bidhaa zako, huko ndiko utaelezea faida na ubora wa bidhaa zako na pia utai link na facebook page yako).

3. Lazima uwe na acount ya EQUIT BANK au benk yoyote yenye uwezo wa kulipia huduma online (hii itatumika kulipia matangazo yako).

Baada ya hapo wewe tayari ni mfanyabiashara mtandaoni.

Kama huna ujuzi huo na unahitaji kufahamu au unatamani kufanya biashara mtandaoni basi usisite kuwasiliana nami nitakusaidia kutimiza ndoto yako.

Tunatoa huduma zifuatazo katika kukusaidia:

1. Tutakutengenezea FACEBOOK PAGE na kukukabidhi ikiwa na followers zaidi ya watu 10,000 (elfu kumi).

2. Tutakutengenezea BLOG ambayo ina muonekano mzuri na tutakufundisha jinsi ya kuitumia.

3. Tutakusaidia ku link blog yako na mitandao ya kijamii.

Kama uko tayari kujitoa kwa ajili hiyo tuwasiliane Whatsapp 0754745798 na uwe mfanyabiashara mtandaoni uone tofauti!!!!

KUWA TOFAUTI NA WENGINE!!!

KARIBU SANA.

PIUS JUSTUS MULIRIYE
0754745798
piusjustus28@gmail.com
www.shuletanzania.info

Friday, March 10, 2017

NJIA MUHIMU SANA UNAZOWEZA KUTUMIA LEO KUTENGENEZA FEDHA KWENYE MTANDAO WA INTERNET KWA WENYE TAALUMA YA UALIMU.




Ualimu ni moja ya taaluma muhimu sana kwenye jamii yoyote. Walimu ndiyo wanaoijenga jamii kutokana na malezi wanayotoa kwa watoto ambao ni kizazi kinachokuja.







Pamoja na umuhimu huu mkubwa wa taaluma ya ualimu, maslahi yamekuwa siyo mazuri. Walimu wamekuwa ndiyo watu wa kulalamika kila siku kuhusu mishahara midogo na kutokuendana na gharama za maisha. Hapo bado hujaangalia wale ambao wamehitimu taaluma hii lakini hawakupata kazi.
Kauli za viongozi wengi zimekuwa ni kwamba kama umekosa kazi au kama kipato hakikutoshi basi jiajiri. Lakini walimu wengi wamekuwa wakilalamika kwamba wao wanawezaje kujiajiri kwa taaluma yao? Mtu atawezaje kwenda kuanzisha shule yake binafsi wakati hana kazi kabisa, au mshahara wake haumtoshi?
Njia rahisi ya kujiajiri au kujiongezea kipato iliyokuwa imezoeleka na walimu ilikuwa kutoa masomo ya ziada kwa wanafunzi maarufu kama tuition, lakini hii pia imepigwa marufuku maeneo ya shuleni.
Hali kama hizi zinawafanya walimu wajione hawawezi kuondoka kwenye matatizo waliyopo. Lakini leo nataka kuzungumza na kila mwalimu ya kwamba ipo njia rahisi ya wewe kujiajiri, itakayokuwezesha kutengeneza kipato cha ziada, bila ya kuacha kile unachofanya sasa.
Njia hii ni kujiajiri na kutoa huduma kupitia mtandao wa intaneti.
Sasa hivi karibu kila mtu mwenye simu anatumia mtandao wa intaneti, na namba inazidi kuongezeka kila mwaka. Hivyo walimu wanaweza kutumia mtandao huu wa intaneti kuweza kutoa huduma kwa wale wenye uhitaji, na baadaye wakaweza kutengeneza kipato.
Kwenye mtandao wa intaneti, unatoa maarifa na taarifa zinazowasaidia watu kufanya maamuzi bora kabisa ya maisha yao.
Kabla ya kuangalia mwalimu anawezaje kutengeneza fedha kwenye mtandao wa intaneti, kwanza soma vitu vitatu muhimu unavyohitaji kuwa navyo ili kutengeneza fedha kwenye intaneti. Visome kwa kubonyeza maandishi haya.

Zifuatazo ni njia kumi(10) anazoweza kutumia mwalimu kutengeneza fedha kwenye mtandao wa intaneti.
  1. Kuandika makala zinazohusu elimu kwa ujumla. Hapa itakuwezesha kujijenga kama mtaalamu wa elimu na hivyo kupata fursa zaidi za kushauri na kufundisha kuhusu elimu.
  2. Kuuza vifaa vya ufundishaji ambavyo umetengeneza au kuandaa mwenyewe. Kama mwalimu unaweza kuwa na notes nzuri ulizoandaa, maswali mazuri na vitu vingine vinavyoweza kutumika kufundisha.Unaweza kuzitengeneza vizuri na kuziuza kupitia mtandao wa intaneti.
  3. Kuandika kuhusu malezi ya watoto. Moja ya vitu ambavyo walimu wanajifunza ni malezi, kitu ambacho wazazi wengi hawajajifunza. Hivyo mwalimu anaweza kuwa anatoa mafunzo ya aina hii na baadaye kuwa mshauri au kutoa mafunzo ya kulipia juu ya malezi bora ya watoto.
  4. Kupata fursa ya kufundisha watoto masomo ya ziada majumbani kwao. Kwa kuwa tuition mashuleni zimekatazwa, mwalimu anaweza kutoa masomo ya ziada kwa kuwafuata wanafunzi kule walipo. Kwa kutumia mtandao wa intaneti, mwalimu anaweza kuwafikia wateja wake wa huduma ya masomo ya ziada.
  5. Kuandaa kozi utakayoitoa kwa njia ya mtandao. Kupitia mtandao wa intaneti, mwalimu anaweza kuandaa na kutoa kozi ambayo watu watajiandikisha na kulipia. Kozi hii inaweza kuhusu mambo mbalimbali yanayoweza kuwasaidia watu.
  6. Kuandika kitabu na kukiuza kwa njia ya mtandao. Kitabu hiki unaweza kukichapa au kukiuza kama nakala tete kama ambavyo ninafanya mimi, ninaandika vitabu mbalimbali na kuviuza mtandaoni.
  7. Kutoa ushauri na mafunzo kwa walimu waliopo vyuoni bado, namna bora ya kusoma na kufaulu mitihani, mambo muhimu ya kuzingatia wanapoanza kazi na hata namna ya kuendeleza na kukuza taaluma zao.
  8. Kuandaa mtaala unaoweza kutumiwa na watu wanaolenga kutoa mafunzo fulani. Kama mwalimu una uzoefu juu ya mitaala, unaweza kutumia uzoefu huo kusaidia wengine wanaoanza kutoa mafunzo mbalimbali.
  9. Kutumia vipaji na uwezo ulionao kutengeneza fedha kwenye mtandao. Hapa unaweza kuandika au kufundisha juu ya vitu vingine unavyojua, ulivyozoea au unavyopenda nje ya ualimu.
  10. Kutumia mtandao wa intaneti kutangaza na kukuza biashara zako nyingine ulizonazo tayari. Kama tayari umeshaanza biashara nyingine, unaweza kutumia mtandao wa intaneti kuzikuza zaidi.
Wakati wa kulalamika kwamba wewe kama mwalimu huna njia za kuongeza kipato zimepitwa na wakati. Una taaluma muhimu sana na zipo njia za bure kabisa kwako kuzitumia kuweza kutengeneza fedha kwa taaluma uliyonayo. Anza kufanyia kazi hayo niliyokushirikisha, na kama utapenda ushauri wangu wa karibu zaidi na hata kukuongoza kwenye hilo, nitafurahi sana kufanya kazi na wewe. Tuwasiliane kwa njia ya wasap namba 0754745798. Karibu sana.
Tumia ujuzi, utaalamu na uzoefu wako kutengeneza kipato kwenye mtandao wa intaneti kupitia SHULE TANZANIA
PIUS J. MULIRIYE
Kocha wa mafanikio, Mwandishi na Mjasiriamali.
Karibu sana kwenye SHULE TANZANIA uweze kutengeneza kipato kupitia mtandao wa intaneti.

NJIA KUMI (10) UNAZOWEZA KUANZA KUTUMIA LEO KUTENGENEZA FEDHA KWENYE MTANDAO WA INTERNET.




Je wewe unatumia mtandao wa intaneti? Una simu ya kupangusa (smartphone) ambayo unaweza kuitumia kutembelea mitandao ya kijamii? Najua majibu yako ni ndiyo, kwa sababu mpaka umesoma hapa, lazima uwe unatumia mtandao wa intaneti.








Sasa swali muhimu zaidi ni hili;
Je umekuwa unatengeneza fedha kwenye mtandao huu wa intaneti kadiri unavyoutumia? Ulishatengeneza hata elfu moja, elfu kumi, laki na hata milioni? Kwa wengi ninaowajua, jibu lao ni hapana. Wao wamekuwa watumiaji pekee, lakini hawajawahi kutengeneza fedha kwenye mtandao huu wa intaneti.
Sasa leo nina habari njema kwako, kama na wewe ni mmoja wa wale ambao wanatumia mtandao lakini hawaingizi kipato kupitia mtandao wa intaneti. Leo nakwenda kukuambia ya kwamba, kwa hapo ulipo sasa, unaweza kutengeneza kipato kwenye mtandao wa intaneti.
Huhitaji kuwa na elimu ya ziada, huhitaji kuwa na mtaji wa kuanzia, wala huhitaji kuwa na vifaa vingi. Unachohitaji tayari unacho, ambacho ni simu yako ya kupangusa (smartphone) na kompyuta kama unaweza kupata.
Je unawezaje kutumia mtandao wa intaneti kutengeneza kipato?
Hapo ndipo pazuri na ndiyo utakachokwenda kujifunza kupitia makala hii, isome mpaka mwisho,
Kwanza kabisa kabla hujafikia kutengeneza fedha, unahitaji kutengeneza vitu vitatu.
Kitu cha kwanza; kuwa kwenye mitandao ya kijamii kibiashara.
Najua upo kwenye mitandao mingi ya kijamii, wasap, facebook, instagram na mingine ya aina hiyo. Lakini sina hakika ni mambo gani unafanya kwenye mitandao hiyo. Huenda umekuwa unafuatilia tu mambo ya watu, huenda umekuwa kwenye timu za kishabiki. Kwa njia hiyo huwezi kutengeneza fedha.


Mfano wa kuwa katika facebook kibiashara.









Ili uweze kutengeneza fedha kwenye mtandao, unahitaji kuwa kwenye mitandao ya kijamii kibiashara. Na hapa unachagua ni huduma gani ya maarifa na taarifa unaweza kuwapa wengine kupitia mitandao ya kijamii unayotumia. Maarifa na taarifa hizi unaweza kuzitoa kutokana na uzoefu ulionao, utaalamu ulionao na hata ujuzi ulionao.
Hivyo chagua mitandao ya kijamii unayoweza kuitumia kutoa maarifa na taarifa. Mizuri kwa kuanzia ni facebook, instagram na whatsapp.
Kitu cha pili; unahitaji kuwa na blog.
Blog ndiyo nyumbani kwako kwenye mtandao wa intaneti. Hapo ndipo watu wanapokutana na kazi zako zote. Kazi zako haziwezi kupotea kama umeziweka kwenye blog yako. Kwenye mitandao ya kijamii zinaweza kupitwa na kusahaulika, ila kwenye blog zitakuwepo milele.
Unahitaji kuwa na blog ambayo utaitumia kutoa taarifa na maarifa uliyodhamiria kuwapa watu ili baadaye uweze kutengeneza kipato. mfano wa blog ni kama huu www.shuletanzania.info
Kama utahitaji kufunguliwa blog na uanze kutengeneza fedha wasiliana nasi Whatsapp 0754745798.

Kitu cha tatu; unahitaji mfumo wa kutunza na kutuma barua pepe (email list).
Watu wanaokusoma na kukufuatilia kupitia mitandao ya kijamii na blog yako, watapenda kusikia zaidi kutoka kwako, hivyo wape nafasi ya kukupa wewe mawasiliano yao, moja wapo email ili uwe unawatumia vitu vizuri zaidi.
Watu hawa wanaokupa mawasiliano yao ni watu ambao wanakukubali na watakuwa tayari kupokea maarifa na taarifa zaidi kutoka kwako. Watumie maarifa na taarifa zaidi kwenye email zao na baadaye utaweza kutengeneza kipato kwenye mtandao.
Ukishakuwa na vitu hivyo vitatu muhimu, sasa unakuja kwenye kutengeneza fedha kwenye mtandao.
Zipo njia nyingi sana za kutengeneza fedha kwenye mtandao kwa kutumia blog. Hapa nitazitaja zile muhimu na nitazielezea zaidi kwenye makala zijazo.
  1. Kutangaza biashara yako na biashara za wengine kupitia mitandao ya kijamii na blog yako.
  2. Kutengeneza maarifa yako kwenye mfumo mzuri na kuwauzia wasomaji wako, kama cd, dvd, kitabu n.k
  3. Kuendesha semina kwa wasomaji wako, kwa njia ya kukutaka ana kwa ana au kwa njia ya mtandao.
  4. Kutangaza huduma zako nyingine kama ushauri.
  5. Kutoa makala za kulipia na watu kuwa wanachama wa blog yako.
  6. Kuuza bidhaa zinazoendana na maarifa unayotoa kupitia mtandao wa intaneti.
  7. Kuweka matangazo ya google na kulipwa kadiri watu wanavyobonyeza.
  8. Kushirikiana na makampuni au mashirika yanayoendana na maarifa unayotoa.
  9. Kutengeneza kundi la mafunzo kupitia mtandao wa whasap.
  10. Kuwaunganisha wasomaji wako na watu wenye huduma ambazo wanazihitaji.
Hizi ni njia za msingi kabisa unazoweza kuanza kuzitumia leo kutengeneza fedha kwenye mtandao.
Tutaendelea kuzichambua moja baada ya nyingine kwenye makala zijazo.
Tumia ujuzi, utaalamu na uzoefu wako kutengeneza kipato kwenye mtandao wa intaneti kupitia SHULE TANZANIA

Kwa msaada zaidi juu ya jinsi gani ufanye ili kutengeneza fedha kwa njia ya mtandao wa internet wasiliana nasi kwa mawasiliano haya;

0754745798-Whatsapp
piusjustus28@gmail.com
JIUNGE NAMI UPOKEE MAKALA KILA IWEKWAPO MTANDAONI