0657128567

Mwanza Tanzania,

Karibu Sana Kwenye Mtandao huu Wa Shule Tanzania

Showing posts with label BIASHARA MTANDAO. Show all posts
Showing posts with label BIASHARA MTANDAO. Show all posts

Friday, August 3, 2018


Moja ya mtaji mkubwa ulionao kwenye maisha ni Upekee wako.Tatizo la wengi ni kuwa wanazaliwa hadi wanakufa hawajajua Kitu cha pekee walichonacho.
~~~~~~~
Kwenye kitabu chao cha “Now,Discover Your Strength”(Sasa,Gundua nguvu yako) waandishi Marcus Buckingham na Donald O. Clifton wanasema kila mtu ana uwezo wa kipekee ambao ni zaidi ya watu Elfu kumi wa karibu yake.
~~~~~~~
Unapogundua eneo lako la uwezo wa Kipekee ndio linaitwa “Strength Zone” yako ambayo unatakiwa kuijua na kuwekeza usiku na mchana hapo.Kozi ya kwanza ninayofundisha wanafunzi wangu kwenye MasterMind Coaching Program ya kila mwezi ni kuijua Strength Zone Yako na jinsi ya kuijenga.
~~~~~~~~~
Uwekezaji wenye faida kubwa duniani ni kuwekeza kwenye Strength zone yako.Kadiri unavyowekeza basi ndivyo Kadiri thamani yako inaongengezeka.
~~~~~~~~~~
Je,Umeshaijua Strength zone yako tayari?

Chukua hatua sasa!

Pius J. Muliriye
Whatsapp | 0754745798

Monday, May 21, 2018

SAIKOLOJIA YA WATU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII

Habari rafiki, natumai unaendelea vizuri na harakati za kukomboa maisha yako na kuelekea katika uhuru wa kifedha.



Katika mfululizo wa mada zetu juu ya jinsi ya kutumia mtandao wa internet kibiashara leo hii ninakuletea mada inayozungumzia Saikolojia ya watu walioko katika mitandao ya kijamii.

Kama tunavyojua, katika mitandao ya kijamii ni sehemu ambako watu hukutana na kujumuika pamoja, kuchati, kuonyesha style mbalimbali za maisha, kwa kulitambua hilo ninapenda kukwambia rasmi kuwa katika mitandao ya kijamii SIO MAHALI PA KUUZIA BIDHAA YAKO AU SIO MAHALI PA KUFANYIA BIASHARA YAKO.

Hii ni sawa na kuwakuta watu wako katika club wanacheza mziki na kuponda raha halafu wewe unaingia na bidhaa zako na kuanza kuwatangazia ili wanunue, nakuhakikishia watakufukuza na hata kukupiga kwa sababu unawaharibia starehe zao.

Kwa hiyo, kama wewe umekuwa ukiweka picha za bidhaa zako kila mahala kwenye mitandao ya kijamii acha mara moja tabia hiyo.

KAMA NDIO HIVYO, NINI UFANYE??

Badala ya kupost picha za bidhaa na kuwatangazia watu wanunue, tengeneza JUKWAA LAKO/KIJIWE CHAKO na huko ndiko utumie kuwaelimisha juu ya umuhimu wa bidhaa unayoitoa na kisha uwauzie, itakuwa rahisi kununua kwa sababu wameshapata elimu juu ya hiyo bidhaa kutoka kwako. Hivyo ndivo unapaswa kufanya.

JUKWAA NI NINI??
Jukwaa katika biashara ya mtandao ni sehemu maalumu ambako unatumia kuwaelimisha watu kuhusu jambo flani. Jukwaa linaweza kuwa;


  • Facebook messenger chat Bot (messenger)
  • Facebook group
  • Whatsapp group
  • Email list 
  • Youtube subscriber etc
Tumia platform hizo kukusanya watu na kisha waelimishe kisha toa ofa yako.

JINSI YA KUJENGA JUKWAA LAKO

Jukwaa linajengwa kwa kutumia software ambazo zinaruhusu watu kuweza kuingia automatically na kisha ujumbe unakuwa unawafata mara kwa mara kulingana na ulivyoset wewe.

Kama utahitaji kujua zaidi na jinsi ya kuweza kujenga na kutengeneza jukwaa lako kitaalamu nimekuandalia kozi maalumu iliyopo kwenye mfumo wa video zikielezea kwa kina hatua kwa hatua jinsi ya kuset program hizo.

Kama utakuwa tayari kujifunza zaidi ili uanze kutengeneza kipato kupitia mtandao basi jaza fomu hii chini tukishapokea fomu yako tutawasiliana na wewe moja kwa moja na tutakupa utaratibu wa kuanza kozi hiyo.





Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako;

PIUS J. MULIRIYE
0717375782 | WHATSAPP
0754745798 | CALL | TEXT

Thursday, May 10, 2018

MILLION 7,885,000/- NDANI YA SIKU 90 KWA KUTUMIA MTANDAO WA INTERNET.

Angalia video hii inayoonyesha jinsi nilivyotumia mtandao wa internet kuingiza hadi 7,885,000/- ndani ya siku 90.

Angalia kisha chukua hatua.


Kama umependezwa na video hiyo na ungependa kujifunza zaidi nakukaribisha kwenye group yetu mpya ya Whatsap kwa kubonyeza picha hii👇


Kama uko tayari kuanza safari hii ya mafanikio tafadhari jaza fomu hii




Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako;

Pius J. Muliriye
0717375782 | Whatsapp only.
www.piusjustus.com

Tuesday, February 27, 2018

DARASA: JINSI YA KUTENGENEZA BIDHAA ZA VIWANDANI.

Habari rafiki mpenda maendeleo, sasa darasa letu liko wazi kwa sasa. Utajifunza utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za viwandani kama vile BATIKI, SABUNI YA KIPANDE pamoja na bidhaa nyigine nyingi.

Kama uko tayari bonyeza HAPA kuingia darasani.


Asante kwa kusapoti kazi yangu, naamini utafanikiwa katika hili.

Wasiliana nasi 
Whatsapp only | 0717375782
           Text only | 0754745798

Sunday, February 25, 2018

JINSI YA KUTENGENEZA BATIKI PART 1

Jifunze jinsi ya kutengeneza batiki kwa njia rahisi kabisa. Kama utapenda kozi hii basi kuna video nimekuandalia mwanzo mpaka mwisho wa jinsi ya kutengeneza batiki aina nyingi ikiwemo Muundo wa sambusa, muundo wa mkeka, bleech, na nyingine nyingi zinakuja. Kuingia darasani bonyeza picha hapo juu itakupeleka moja kwa moja kwenye darasa letu. 

Unaweza kusikiliza utangulizi wa kozi yetu hapa chini.


Bonyeza hapa kuingia darasani www.piuscollege.wordpress.com


Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako.
PIUS J. MULIRIYE
Whatsapp tu | 0717375782

Friday, February 23, 2018

MISINGI (3) YA KUWEKA JUHUDI KUFIKIA MAFANIKIO YAKO.


Nafahamu ya kwamba kila mmoja anafanya mambo mbalimbali kama vile kusoma, kufanya biashara, na kutoa huduma mbalimbali. Lakini yote hayo huleta  matokeo chanya  endapo utaweka juhudi za kweli katika endaji wako na kinyume cha hapo utakuwa unashindwa. 

Watu wengi huwa tunafanya vitu ili mradi tu, siyo kama tunapenda kufanya vitu hivyo ila kwa kulazimishwa tu au kwa kuiga kutoka kwa watu wengine mwisho wa siku tunajikuta hatufanyi tena vitu hivyo.

Hebu tuendelee kidogo tuone maana ya neno JUHUDI ni kile kitendo cha kufanya kitu  kwa kutumia bidii, maarifa, nguvu na umakini wa hali ya juu ili kupata matokeo sahihi. Pia juhudi ni maarifa, njia, nguvu ambayo unaipata hata pale wanaokusaidia kwa sasa wakikuucha  je, unauwezo wakusimama peke yako?

Mfano wewe ni mwanafunzi wazazi au ndugu zako wanakusomesha kwa hali na mali, swali la kujiuliza wewe mwanafunzi je una uwezo wa kusimama peke yako endapo wanaokusaidia watakuacha? Je utatumia juhudi gani katika kutafuta njia zako binafsi za kukamilisha jambo fulani?
Ifuatayo ndiyo misingi ya kuweka juhudi katika safari yako ya mafanikio;

Kwanza, Kujitoa.

Ili kuona unapata mafanikio makubwa hakikisha ya kwamba unajitoa kwa moyo wote katika kupata kile unachokihitaji. Kwa kitu chochote unachofanya jitoe kukipenda kitu hicho. Kwa mfano wewe ni mfanyabiashara eneo fulani hakikisha unaipenda kazi yako kwa kujifunza kila siku vitu vipya juu ya jambo unalolifanya. Pia kwa jambo lolote unalolifanya weka juhudi zote na kuhakikisha utapata kile unachokihitaji.

WEKA JUHUDI KWENYE KAZI ZAKO BILA KUCHOKA.

Pili, uvumilivu.

Wengi wetu huwa hatuna chembe ya uvumilivu hata kidogo hasa pale changamoto zinapojitokeza katika mambo tunayofanya. Pia tukumbuke ya kuwa changamoto ni sehemu anayopitia mtu yeyote msaka mafanikio. Jambo la msingi la kuzingatia ni uvumilivu na siyo kukata tamaa. Kuna usemi wa wahenga unasema ‘mvulivu hula mbivu’ Hivyo tuishi usemi huu kwa kufanya kazi kwa bidii na kuzikubali changamoto na kujua jinsi gani ya kuziepuka ili tupate mafanikio tunayoyahitaji.

Tatu, kuwa mbunifu.

Hii ndio siri kubwa katika kutafuta mafanikio makubwa ambayo  yapo upande wako. Kuwa mbunifu katika mambo mbalimbali huku ukiyatendea kazi hayo uliyoyabuni kwa juhudi zote. Kama wewe ni mwanamziki basi fanya kazi hiyo kwa juhudi zote huku ukiamini ya kuwa kipaji hicho ndio sehemu ya maisha yako na kipato chako, usifanye kitu kwa kujaribu.
Katika suala la kuwa mbunifu kuna msomi mmoja amewahi kusema ya kuwa dunia ya leo haitaki kujua wewe una nini ila ioneshe dunia wewe una nini? Nafikiri kwa mfano huo utakuwa umenielewa vizuri zaidi. Pia tukumbuke ya kuwa ubunifu sio lazima kuvumbua kitu kipya bali hata kwa kukiongezea ubora kitu cha zamani pia ni ubunifu pia.

Wapo baadhi ya watu wana pesa  lakini hawana juhudi. Kama wewe ni miongoni mwa watu hao kumbuka pesa hizo zitakuwa ni za msimu na pindi zitakapoisha utabaki unashanga tu. 

Watalamu mbalimbali wamebaini ya  kuwa na pesa bila  juhudi sio kufikia malengo. Tenda mambo yako katika mtiririko unaoelewaka na ambao unaweza kuutimiza kwa muda muafaka , ukifanya hivyo kuwa tayari kuyapokea mafanikio makubwa.

Ewe rafiki yangu, tukumbuke ya kuwa JUHUDI ndio msingi rasmi wa mafanikio ambayo unayahitaji. Swali la kujiuliza je, upo tayari kulifanya jambo hilo kwa juhudi dhabiti? Kama jibu lako ni ndio basi weka juhudi zako zote katika utendaji wa jambo fulani kwa kuzingatia muda. Ukifanya hivyo mafanikio makubwa yatakuwa upande wako siku zote.

MUHIMU:


Je unapenda kujishughulisha na ujasiriamali???
Kama ni ndio, nimekuandalia kozi maalum kwa ajili yako wewe unayependa kujiongezea kipato.
Kozi hiyo inafundisha jinsi ya kutengeneza batiki zenye ubora mkubwa sana. Kozi hii itafanyika mtandaoni.
Kama unatamani kujiunga basi wasiliana nami whatsapp 0717375782 nikupe maelekezo zaidi.
Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako.
PIUS J. MULIRIYE
0717375782 | Whatsapp tu.
0754745798 | meseji tu.
piusjustus28@gmail.com

Thursday, February 22, 2018

MAMBO NANE (8) MUHIMU SANA YA KUFAHAMU KABLA YA KUTENGENEZA BATIKI.

Habari rafiki yangu, naamini unaendelea vizuri na mapambano ya kuboresha maisha yako.

Kama ilivyo kawaida yangu nakufunulia fursa mbalimbali ambazo ukiamua kuchukua hatua unaweza kubadili maisha yako kabisa. Cha msingi sana ni kuchukua hatua.

Leo nakuletea fursa ya kutengeneza batiki, fursa ambayo si wengi sana wanaijua kwa maana ya jinsi ya kutengeneza, hata kama watu wanajua kutengeneza bado hawachukui hatua na kufanya fursa hii kuwa ya wachache na imewatajirisha wengi sana na wengine maisha yao yamebadilika kabisa.

Nisikuchoshe sana ndugu, leo hii nakuletea list ya vitu muhimu au mambo manane (8) ya muhimu kuyajua kabla ya kuanza kutengeneza batiki yenye ubora wa hali ya juu. Vitu hivyo ni:-

MAHITAJI:
1.Vibao vyenye urembo mbalimbali.
2.Sponji zenye urembo mbalimbali.
3.Brash kubwa/ndogo.
4.Meza kubwa yenye urefu wa mita moja mpaka mbili.
5.Sufuria.
6.Vitambaa
7. Jiko.

MADAWA:
8.Sodium hydrosulphate.
9.Caustic soda
10.Mshumaa.

KAZI ZAKE:
1.Sodium hydrosulphate ni kuimarisha rangi isichuje,kama itachanganywa na caustic soda.Madawa haya huwa kazi yake ni moja lakini ikikosekana moja nyingine haifanyi kazi.
2.Kazi ya mshumaa ni kuweka urembo kwenye nguo au kwenye vitambaa kwa kutumia vibao au sponji zenye urembo wa tembo,twiga,matunda au aina yoyote ya urembo unayotaka mtengenezaji.

Zifuatazo ni picha za baadhi ya batiki ambazo ninatengeneza na kuwauzia wateja wangu.

















Je unatamani kujua kutengeneza batiki?? Hii ni miongoni mwa fursa zilizojificha kabisa na watu hawazioni na hata kama wanaziona hawachukui hatua yoyote, kama unasoma makala hii na unasikia moyoni unatamani kujua jinsi ya kutengeneza batiki hizi basi naamini ndani ya muda mfupi unaenda kuwa mtu mwingine kabisa.

Inawezekana kabisa unajiuliza kuhusu mtaji inagharimu kiasi gani, nataka nikutoe hofu, mtaji wake ni kiasi kidogo saaaana ambacho huwezi kuamini, na utajiuliza kwa nini watu hawafanyi biashara hii kwa wingi na wakati mtaji ni kiasi kidoooooogo sana, nimeshasema sababu hapo juu ni kwamba watanzania wengi hatupendi kujishughulisha, tunapenda kukaa vijiweni kulalamika maisha magumu tu na kuzungumzia maisha ya watu. Ninaamini baada ya kusoma makala hii utakwenda kuchukua hatua mara moja.

Nina habari njema kwa wewe ambaye umependa kujifunza mradi huu.

Kama uko serious na unataka kujifunza jinsi ya kutengemeza batiki basi nimekuandalia kozi maalumu kwa ajili yako.
Kozi hiyo itakufundisha kwa kina, hatua kwa hatua jinsi ya kutengeneza batiki yenye mikunjo/michoro mbalimbali ya kupendeza machoni pa watu.

Kozi hiyo itakuwa kwa njia ya VIDEO ambayo itakusaidia kuangalia kwa vitendo jinsi tunavyokunja mikunjo hiyo na kuweka rangi mbalimbali.

Je uko tayari???

Kama uko tayari niandikie ujumbe whatsapp 0717375782 kwamba uko tayari kujifunza BATIKI kwa njia hiyo kisha nitakuingiza darasani. KARIBU SANA.

Najua bado unajiuliza mtaji ni shilingi ngapi???? Najua vijana wengi tukitaka kuanza mradi flani tunawaza sana kuhusu mitaji. Nataka nikwambie kwa mradi huu hata sh. 15,000/- unaweza kutengeneza batiki nzuri na watu wakabaki kukushangaa. Pia utakuwa unajiuliza nitatoa wapi malighafi???? nataka nikutoe hofu, Tanzania sasa ni ndogo sana, kama hutapata sehemu au mkoa uliopo tutakutumia popote ulipo ilimradi tu utimize ndoto zako. Usiogope, chukua hatua sasa, natamani sana kukuona darasani.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako;

Pius J. Muliriye
0717375782 | whatsapp tu.
0754745798 | meseji tu (usipige)
piusjustus28@gmail.com
www.piusjustus.com

Tuesday, February 20, 2018

NJIA TANO (5) BORA ZA KUKUZA BIASHARA YAKO.



Moja ya changamoto kubwa inayowakumba wafanyabiashara walio wengi ni kutokujua kiundani juu ya biashara zao. Kutokana na changamoto hiyo ya kutokujua kiundani biashara zao, wafanyabiashara hao walio wengi hujikuta biashara zao huwa haziwi za muda mrefu na hata pale zinapokuwa za muda mrefu huwa hazikui.
Naamini kwa kuwa lengo lako ni kukuza biashara, ni vyema kwa kupitia makala haya, ukafahamu pia baadhi ya mambo muhimu yatakayokusaidia kukuza hata biashara yako. Nakusihi ufuatane nami mwanzo hadi mwisho ili kuweza kuona biashara yako inakuwa na maisha marefu na yenye kukua siku hadi siku.
  1. Ongeza maarifa kwa kujifunza.
    Kama kweli unahitaji mafanikio zaidi ya kiabiashara ni vyema ukawa ni mtu wa kujifunza kuhusiana na biashara yako. Ni lazima ujifunze mbinu mbalimbali ambazo wanazitumia wafanyabiashara wengine kufanikiwa. Kujifunza huku kukupe muda muafaka wakugundua pale ambapo wafanyabiashara wengine wanashndwa. Baada ya kujua wanashindwa wapi kwako ifanye kama fursa ya kuboresha biashara yako. Kufanya hivyo kutakufanya uongeze wateja kwani utakuwa mbunifu zaidi.
Acha kuridhika na hali uliyonayo.
  1. Badili tabia zako.
    Moja ya chachu nzuri ya kukufanya ukue kibiashara ni lazima uweze kujua vizuri tabia yako. Inawezekana wewe unajiona upo sawa ila kumbe sivyo unavyofikiri. Hata hivyo ili kuweza kujua ni ipi tabia yako ni vyema ukafanya uchunguzi ili kujua watu wanakuzungumziaje wewe? Kufanya hivyo kutasaidia kwa sababu watu wengine ndio wana picha kamili juu ya wewe na biashara kwa ujumla. Pia ili kuweza kufanikiwa ni lazima uweze kubadili tabia uliyonayo ya uvivu na ongeze juhudi za kiutendaji katika kufanya kazi.
    3. Tenga muda wa kufikiri kuhusu biashahara yako.
    Moja ya mbinu ya kuweza kukuza biashara yako ni kuweka muda kwa ajiri ya kujua biashara yako inakwenda vipi. Biashara zilizo nyingi huwa hazina maisha marefu kwa sababu wahusika hawa na muda wa kutosha kuhusu kufikiri jinsi gani biashara inakwenda bali walio wengi hutazama faida tu. Kufanya hivyo tambua biashara yako hatakuwa na Maisha marefu ni vema ukawa mzuri kujua utendaji wako wa kibiashara na changamoto zake na jinsi ya kutatua.
    4. Tambua mchango wako wa watu wengine.
    Ukitaka kufanikiwa zaidi ni vyema ukajua ni kwa jinsi unavyojenga mahusiano mazuri pamoja na wafanyabiashara wengine  na wateja wako pia. Mchango mzuri uliona nao utakufanya uongeze wateja wengine. Kwa mfano unauza biashara fulani ghafla ukaishwa bidhaa fulani harafu mteja akaja kuuliza bidhaa hiyo, usimwambia mteja huyo kwamba kama huna bidhaa hiyo mwambie ngoja nikakuchukulie kwenye stoo. Na kwa kuwa wewe huna bidhaa hiyo nenda kwa jirani yako nenda ukanunue na uje kumpa mteja huyo. Kufanya hiyo kutakufanya uweze kujenga mahusino na wafanyabiashara nyingine pia njia ya kuongeza wateja na kufanikiwa zaidi.
    5. Usiridhike na hali uliyonayo.
    Kuwa mfanyabiashara mkubwà ni lazima kuwa katika imani ambayo inatamani kufanikiwa zaidi. Maana yangu hata kama wewe unajiona tayari umefanikiwa wewe jione bado una kiu ya kufanikiwa zaidi. Kama wasemavyo kwamba pesa haitoshi basi hata wewe una deni la kufanikiwa zaidi. Moja ya kufeli kwa biashara ni pale mtu anapoona amepata mafanikio na yeye anaridhika . Kuridika ni adui wa mafanikio. Kuridhika ndiko kunako turudisha nyuma watu wengi sana. Pia nikumbushe ya kwamba kufeli sio kushindwa ni sehemu ya mafanikio.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako. 
Kama unataka kujifunza jinsi ya kutengeneza bidhaa mbalimbali za viwandani kama vile BATIKI, SABUNI, CHAKI, SHAMPOO n.k. kwa njia ya mtandao basi tembelea www.piuscollege.wordpress.com


Wasiliana nasi Whatsapp (only) | 0717375782


JARIBU TENA


DUNIA INA FURSA NYINGI SANA


Friday, February 16, 2018

FANYA HIVI KUGUNDUA KIPAJI CHAKO.

Moja ya changamoto kubwa inayowakabili watu wengi ni kutojua kwa undani kipi  kipaji chako ambacho Mungu amekupa na ambacho unaweza ukakitumia kwa namna moja ama nyingine ili uweze kuleta mabadiliko chanya katika jamii na wewe binafsi.


Na kwa kuwa kuna watu wengi ndio wapo kundi hilo, kuna usemi unasema ya kwamba wengi wape basi ngoja nifanye hivyo kuweza kuwapa somo hilo la namna ya kujua kipaji chako  kwani hii itamsadia kila mmoja ambaye atakwenda kufuatana nami mwanzo hadi mwisho katika mukutadha wa makala haya.
Tunapozungumzia neno kipaji huenda kila mmoja akawa na maana yake ambayo anaifahamu, lakini kwa namna moja ama nyingine ni lazima mtu aweze kuzaliwa nacho hivyo Mwenyezi Mungu huhusika pia katika kumpa mtu kipaji.
Hivyo endapo mtu atakifahamu kipaji chake inampasa sasa ajue namna ya kukiendeleza kipaji hicho ili kisife. Pia ikumbukwe ya kwamba tunapozungumzia kipaji tunamzungumzia binadamu na maisha yake kwa ujumla.
Katika tafiti ambazo zimewahi fanywa na  Dr. Fred Luskin kutoka Stanford university yeye aliweza kugundua ya kwamba asilimia 65 ya watu wengi hawajui vipaji vyao na katika kundi kubwa la idadi hii ya watu ndio ambao wanafanya vitu ambavyo sio vyao.
Na pia  asilimia 35 iliyobaki hawa ndio ambao wameweza kuvijua hivyo vipaji vyao ingawa haviwasadii katika maisha yao na wengine kwa asilimia 100, hii ni kutoka mafanikio yatokanayo vipaji hivyo huwa ni ya muda mrefu.
Hivyo kwa kuwa watu wengi tunataka mafanikio ya muda mfupi uvumilivu hufika ukomo na kujikuta tunaviacha vitu hivyo na kuingia kufanya vitu vingine.
Mfano mtu anakuwa na kipaji cha kucheza mpira katika timu kubwa hapa nchini na nje ya nchi,na kwa kuwa huenda amecheza kwa muda mrefu bila matarajio yake kutimia mtu huyo huacha kile ambacho hukifanya na kuamua kufanya kitu kingine ambacho sio kipaji chake mwishowe mtu huyo anajikuta anafanya hiki anakiacha mara kile nacho anakiacha.
Ukiona hicho unachokiita kipaji chako hakitoi burudani, hakifundishi, hakishangazi basi hicho sio kipaji.
Namna ya kugundua kipaji chako.
  1. Kumuomba Mungu.
Hapa huwa pananifanya nimkumbuke sana rafiki yangu Samweli Salali kwani aliwahi kuniambia ya kwamba kipaji ni kusudio la Mungu kwa kila mja wake. Kwani katika mafundisho yake katika vitabu vya dini vinasema kabla sijaumba nilikujua.
Hii inamaana kila mwanadamu aliyeumbwa na Mungu ana kipaji chake, hivyo kinauwezo mkubwa wa kubadili maisha yake na jamii kwa ujumla, ila kipaji hicho watu wengi hawahujui mpaka dakika hii kuwa kipi kipaji chake ambacho Mungu kampa.
Hivyo kama wewe ni miongoni mwa watu hao ni muda wako muafaka wa kutumia Muda huu kumuomba Mungu akuonyeshe kipaji chako hasa na kipi kwa sasa?

  1. Marafiki, ndugu na wazazi.Hili ni kundi muhimu sana ambalo litakusaidia wewe kujua kipaji chako. Labda unaweza ukajiuliza ni kivipi? Tulia leo nipo kwa ajili yako. Watu ambao wanakuzunguka ndio wana picha kamaili juu ya maisha yako.
Kwa mfano mtu akiwa mlevi hawezi kusema mimi ni mlevi ila watu ambao wanakuzunguka ndio ambao watasema yule jamaa ni mlevi sana. Picha hiyohiyo ya kumuona mtu mwingine tabia yake ndiyo ambayo inatumika kujua kipaji chako.
Hebu waulize nyie mnanionaje, mna picha gani? Mnahisi nina kipaji Gani? Baada ya kuwauliza hayo wao ndio watakupa picha kamili juu ya kipaji chako na maisha yako kwa ujumla.

3. Matatizo.
Matatizo ni njia nzuri ya bora sana ya kugundua kipaji chako. Ulimwegu wa leo ni ulimwengu wenye changamoto nyingi sana, hata hivyo kutokana na suala hilo, pale matatizo yanapotokea na kuyapatia ufumbuzi sahihi hapo ndipo utakapojua kipaji chako.
Kwa mfano watu wengi leo hii wanapenda maisha ya kufanyiwa kila kitu. Tuchukulie leo hii unamtegemea mtu fulani ili aweze kukutimizia lengo lako. Halafu siku ya siku mtu huyo anakufukuza nyumbani kwake na kukuambia nenda kajitegemee.
Baada ya kuambiwa hivyo ndipo unakuja kugundua ni kipi kipaji chako baadala ya kuendelea kuwa tegemezi. Hebu tuone mfano mwingine unakuta mtu alikuwa ni mfanyakazi wa ofisini ila baada ya kustafu unajikita katika ufugaji mwisho wa siku unagundua wewe ulikuwa una kipaji cha ufugaji badala ya kufanya kazi za maofisini.
Hivyo wito wangu kwako ni vyema ukagundua kipaji chako mapema usisubiri changamoto fulani zitokee ndipo ugundue kipaji chako.
  1. Mashindano.
Kuna baadhi ya nchi huandaa mashindano mbalimbali kwa ajili ya kusaka vipaji, hili jambo jema sana hata hapa kwetu nchini kuna baadhi ya mashindano hufanyika ambayo husaidia kujua vipaji vya watu kama vile bongo star search, fiesta, DJ compition, umiseta na mangineyo mengi.
Hivyo kama kweli unataka kujua kipaji chako endapo yatatokea mashindano yoyote yale jitahidi sana kwenda kushiriki kwani hii itakusaidia kwa kiwango kikubwa kuweza kujua ni kipi kipaji chako.
Mpaka kufikia hapo niweke nukta kwa kusema kama ukwisha kugundua hicho kipaji chako ni vyema ukajua ni namna gani ya kugeuza hicho kipaji chako kuwa pesa, kwani hapo ndipo palipo kuwa na changamoto kubwa.

Tuesday, February 13, 2018

TUNAISHI KWENYE DUNIA YENYE FURSA

Monday, February 12, 2018

MAPINDUZI KATIKA BIASHARA YA MTANDAO


Thursday, February 8, 2018

HII NDIO BIASHARA INAYOLIPA KULIKO ZOTE

Habari rafiki,
nimekuwa nikiulizwa ni biashara gani ambayo ninaweza kumshauri mtu afanye ambayo inalipa sana kuliko zote, na hili ndio jibu sahihi, chukua muda kutazama video hii.

Wednesday, February 7, 2018

MATATIZO YAKO YAWE CHANGAMOTO YAKO


Sunday, January 21, 2018

KOSA UNALOLIFANYA KATIKA BIASHARA YAKO

Habari rafiki, natumaini uko salama kabisa na unaendelea vizuri na harakati za kuboresha maisha yako.



Leo nahitaji kukupa tip moja muhimu sana katika biashara yako.

Nimekuwa nikisikia watu wengi wakisema biashara zao hazitoki, hazifanyi vizuri sokoni na wengine wamefikia hatua ya kusema biashara zao ni mbaya ndo maana hazinunuliwi.

Leo nataka nikwambie, bidhaa yako ni nzuri sana na jamii inaihitaji sanaaa, tatizo kubwa kwa watu wengi hawajui kufanya masoko (MARKETING).
Nimekuwa nikiona watu wakipost picha za bidhaa zao mtandaoni na bado wanashangaa kwanini watu hawanunui na wakati tangazo lake limeonekana na watu wengi.

Ukitaka kutangaza bishara yako mtandaoni ujue kabisa kuna Formula ambayo inatumika kutangaza biashara mtandaoni na kupata wateja wengi sanaaa.
Siri kubwa ya kufanikiwa mtandaoni jaribu kujifunza sana, acha uvivu, gharamia elimu hiyo utaona matunda yake.

Kama utajitaji nikushike mkono katika kutumia mtandao kufikia watu wengi sana mtandaoni basi wasiliana nami whatsapp 0754745798 tuzungumze na nitakusaidia kufanya hivo.
Asante sana.
Ni mimi ninayejali mafanikio yako.


PIUS J. MULIRIYE
0754745798-Whatsapp

Monday, January 15, 2018

USHUHUDA WA WALIOJARIBU KUFANYIA KAZI MAFUNZO YA KITABU CHA MILIKI KIWANDA MILIKI UCHUMI.

Habari rafiki yangu mpenda maendeleo, naamini uko vizuri na unaendelea na harakati za kuboresha maisha yako.

Leo napenda kukuletea shuhuda za baadhi ya watu ambao wamepata elimu ya utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za viwandani kupitia kwenye kitabu changu cha MILIKI KIWANDA MILIKI UCHUMI na wamefanikiwa kutengeneza products hizo na wamenitumia picha za bidhaa zao na kunipongeza kwa kuwasaidia kufikia hatua hiyo.

Picha zifuatazo ni baadhi ya picha ambazo nimetumiwa, ziangalie na wewe uhamasike kujaribu kutengeneza bidhaa yako, huwezio jua kesho unaweza kutengeneza bidhaa ikawa maarufu na ikawa ndo biashara yako na ikakutoa kimaisha

Asante sana kaka, namshukuru Mungu kupitia kitabu chako nimeweza sasa kutengeneza sabuni ya mche na ina povu jingi sana na imeanza kupendwa sana na watu wanaonizunguka. Nashukuru kwa kunisaidia kupata kazi kwani nimehangaika muda mrefu bila ajira na sasa nimepata cha kufanya naamini itanirahisishia maisha kabisa. Asante sana na Mungu akubariki.

" Kaka nimejaribu kutengeneza sabuni kulingana na maelekezo niliyoyapata kwenye kitabu chako  cha MILIKI KIWANDA na sasa nimeweza kufanya vizuri na nategemea nikirudia nitazidi kufanya vizuri zaidi. asante sana na Mungu akubariki kwa kazi yako ya kuelimisha umaa"
Kaka hii ndo kazi yangu, nimefanikiwa kutengeneza na iko vizuri sana, tatizo liko kwenye kukata sabuni, naomba usichoke kunielekeza, natamani kufanya zaidi ya hapa. Asante sana kwa msaada wako, kitabu chako kimekuwa na msaada mkubwa sana.
Kaka wewe ni mtu hatari sana, natamani watanzania wote wangeweza kujifunza kutoka kwako, umenisaidia sana na sasa ninaanza kuingia sokoni na sabuni yangu imekaa vizuri sana, Mungu akubariki sana ndugu yangu.
 
Kaka nashukuru sana kitabu chako kimenisaidia sana na sasa nimeanzakutengeneza sabuni ya Unga na imetoa povu jingi sana mpaka nimejidharau sana, kumbe mambo haya huwa yanawezekana mtu kutengeneza mwenye we nyumbani, nashukuru sana umenipatia ajira. Mungu akubariki sana Kaka.

Hizo ni baadhi ya shuhuda za watu ambao wamejaribu kufanyia kazi walichokisoma kutoka kwenye kitabu changu cha MILIKI KIWANDA MILIKI UCHUMI. 
Naamini siku si nyingi tutakuwa na watu wanamiliki viwanda vyao nyumbani kwao na watakuwa wanatengeneza pesa bila shida kabisa. Kama na wewe ungependa kujifunza ujuzi huo, basi huna budi kupata copy yako ya kitabu hiki, kitakusaidia sana na baada ya hapo tuendelee kuwasiliana ili tuweze kusaidiana pale unapokwama.

kama unapenda kupata kitabu hicho, basi BONYEZA HAPA kukipakua kitabu hicho.

Asante sana na nikutakie siku njema katika kupiga vita umaskini.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako;


PIUS JUSTUS MULIRIYE
0754745798



Sunday, January 14, 2018

MAMBO MATANO YA KUJUA KABLA YA KUAMUA KUJIAJIRI.

Habari rafiki wa piusjustus.com;

Leo nimekuletea makala kwa njia ya video itakayokufundisha jinsi sahihi ya kujiajiri. Na hays ndio mambo muhimu matano (5) ya kujua kabla ya kuamua kujiajiri.

Karibu usikilize!!





sasa unaweza kupakua app yetu ili uwe wa kwanza kupata makala na video zinapowekwa mtandaoni. Bonyeza hapa kuipakua PIUS JUSTUS APP

Ni mimi mwenye kujalia mafanikio yako;


PIUS JUSTUS MULIRIYE
0754745798-whatsapp


Sunday, October 22, 2017

JINSI YA KUTENGENEZA PESA MTANDAONI KWA NJIA RAHISI KABISA.

Habari rafiki, Natumai unaendelea vizuri na harakati za kuboresa maisha yako.

Leo hii nakuletea somo muhimu sana ambalo wengi wanatamani kulijua lakini hawako tayari kulitafuta kwa nguvu zao zote kwa kuogopa gharama ambazo wanaweza kuzitumia kupata elimu hiyo.

Je wewe ni mmoja wa watu ambao wanatamani sana kutengeneza kipato cha ziada kupitia mtandao unaotumia kila siku? kila siku unatumia pesa kuingia kwenye mitandao tofautitofauti bila ya kujua unapoteza muda na pesa zako bila ya wewe kujua. Nimejitoa kuwasaidia watu wa namna hiyo ambao hawajui ni njia gani wazitumie kuingiza kipato kupitia mtandao ambao wanautumia kila siku.

Mimi niliamua kuchukua hatua na sasa ninatengeneza kipato takribani kila siku. Utajisikiaje kila siku unapigiwa simu kila siku watu wanaomba huduma yako na wanakulipa? je unajua mimi nafanyaje?

Kama unataka kujua hayo basi endelea kuwa na mimi nitakuonyesha hatua kwa hatua.

Kwanza kabisa nikukaribishe uweze kupata kozi ambayo nimekuandalia hapa mtandaoni naamini itakufungua sana na hapo ndio itakuwa njia yako ya mafanikio katika kufanya biashara mtandaoni.

Angalia video hii kisha chukua hatua mara moja. BONYEZA PICHA HII KUONA VIDEO HIYO.


Baada ya kozi hiyo niandikie kama utakuwa na swali lolote kupitia email yangu piusjustus28@gmail.com au whatsapp 0754745798 nitaendelea kukusaidia.

Kaa tayari kwa masomo mengine mengi kuhusu kozi hizi.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako.


PIUS JUSTUS MULIRIYE
0754745798
piusjustus28@gmail.com


Wednesday, October 18, 2017

UKWELI KUHUSU KUPATA PESA MTANDAONI.

Habari rafiki yangu, naamini unaendelea vyema na kuboresha maisha yako.











Leo nataka nikushirikishe kitu muhimu sana ambacho kitaweza jubadilisha mtizamo wa baadhi ya mambo ambayo ulikuwa ukiyafikiria ni kweli kumbe sio kweli.

katika dunia ya sasa kuna mambo mengi sana ambayo yamekuwa yakikuwa kwa kasi ikiwemo matumizi ya mitandao ya kijamii, naamini wewe ni mmojawapo wa watumiaji wa mitandao hiyo.

Katika mitandao watu wanafanya biashara zao na zinakuwa kwa kasi kabisa na wanapata vipato vikubwa sana, na kuna wengine hawajui kama unaweza kupata kipato kikubwa sana kwenye mitandao ya kijamii.

Kuna wengine wamekuwa wakijua kuwa ni rahisi kupata fedha kwa kutumia mitandao na wanachokijua ni kwamba ukipost kitu chochote kile na watu waka click basi kuna kiasi cha MB zinaingia kama hela kwenye akaunti yake.

Ukweli ni kwamba, katika ulimwengu wa biashara ya mtandao hakuna kitu kama hicho na wala hakitakuja kutokea, unachotakiwa kujua ni kwamba ili upate pesa mtandaoni ni lazima ufanye kazi ya ziada ambayo mwisho wa siku itakulipa vizuri sana.

Mimi nimenufaika na matumizi ya mtandao kukuza biashara yangu na sasa nianaingiza kiasi flani kila siku, na hii imetokana na kujifunza kuhusu mtandao na kufanyia kazi.

Nikuuize swali tu, utajisikiaje unapopigiwa simu na mtu anataka akulipe kwa huduma unayotoa? au utajisikiaje unaamka asubuhi unakuta akaunti yako ya mtandaoni imeingiza kiasi flani cha fedha?

Naamini utajisikia vizuri sana.
Kaa nami na tembelea mtandao huu kila siku ili upate kujua namna sahihi ya kufanya ili uweze kuongeza kipato chako kupitia mtandaoni.

Tumia mitandao ya kijamii kwa faida.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako.


Pius J. Muliriye
0754745798
0657128567
piusjustus28@gmail.com
JIUNGE NAMI UPOKEE MAKALA KILA IWEKWAPO MTANDAONI